Kanisa Hai la Mungu

Utume wa Biblia

Zaidi ya asilimia 25 ya Biblia ni unabii. Mungu alitumia manabii Wake wa kweli, kama ilivyo nakiliwa katika Biblia yako, kuonyesha mapenzi Yake na mpango Wake kwa watu wa kale wa Israeli na mataifa mengi ya jirani. Manabii walikuwa watumwa wa Mungu. Walitoa maelezo na ufunuo.  Kamusi ya Biblia ya Unger inatoa maoni juu ya dhima ya manabii, “ Sehemu iliobashiriwa ilikuwa ni ya mara kwa mara katika maudhui ya ujumbe wa nabii. Lakini hii siyo sehemu pekee. Mara nyingi Manabii wana dhima ya waleta marekebisho katika jamii na siasa,  wahubiri wa kusisimua ambao ni waadilifu na wafufuaji wa dini, pamoja na kuwa watabiri  wa hukumu au baraka, kufuatana na wakati unavyo dai. Ujumbe wa nabii ulikuwa daima wa kidini na kiroho, ukiwatangazia wanadamu mapenzi ya Mungu kwa na kuwaita wamtii kabisa” (uk. 893).

Manabii wa kweli wa Mungu, walinakili katika Maandiko, na kufumbua mipango Yake
kwa binadamu. Vile vile walitoa onyo la Mungu kwa watu wa kale wa Israeli, na mataifa mengine mengi. Kwa mfano, baada ya kifo cha Jehoiada mfalme wa Yudah, taifa lilimuasi  Mungu wa kweli na kuabudu masanamu: “Kwa hivyo wakaacha nyumba ya Mwenyezi Mungu wa baba zao, na kutumikia sanamu za mbao na miungu; na gadhabu ikaangukia Judah na Yerusalemu kwa sababu ya dhambi zao” (2 Mambo ya Nyakati 24:18).

Kote katika historia, wengi wamefuata kimakosa miungu na manabii wa uongo. Tunapashwa kuwa waangalifu. Tunawezaje kumtambua nabii wa uongo? Ikiwa kama leo mtu anadai kuwa nabii, lakini ana sema kinyume na maneno ya wazi ya Maandiko, kwa kuweka maneno yake mwenyewe juu ya imani “kwa wale walio kombolewa” (Yuda m. 3), ni nabii wa uongo. Watumishi wa Mungu wanahubiri na kufunza kufuatana na neno Lake, Biblia! Hya pia yanahusu unayo soma katika Tovuti hii! Tujaribu, thibitisha maneno yetu katika Biblia yako, na hakikisha kuwajaribu wengine wanaosema kwamba wanafunza neno la Mungu.

Unabii wa Biblia unaonya watu na mataifa kutubu, ili wajiepushe na adhabu na kushuhudia baraka Zake. Katika kitabu cha Ufunuo, Yesu Kristo anaahidi kulinda wale walio waaminifu. Katika barua kwa Kanisa la Philadelphia, Mtume Yohana ananakili ujumbe huu. “Kwa kuwa wewe umezingatia agizo langu la kuwa na uvumilivu, nami pia nitakutegemeza salama wakati ule wa dhiki inayoujia ulimwengu mzima kuwajaribu wote wanaoishi duniani ” (Ufunuo 3:10). 

Sio tu kwamba Manabii wa Mungu wameita mataifa yao yajirekebishe na kuondokana na uovu; ila wame funua mpango wa Mungu wa siku za mbeleni. Somo muhimu la unabii wa Biblia  ni kwamba utawala uliyo mikononi mwa binadamu  utaishia katika mangamizo ya moja kwa moja. Kama Yesu alivyosema katika Mathayo 24:22, “Kama siku hizo hazingalipunguzwa, hakuna binadamu yeyote ambaye angeokoka; lakini siku hizo zitapunguzwa kwa ajili ya wale walioteuliwa.”

Unabii wa Biblia unatuambia kwamba wakati wa kuerekebishwa unakariabia katika sayari yetu. Mtume Petro aliandika kuwa Mungu ata, “…waletea yule Kristo aliyemteua ambaye ndiye Yesu, ni lazima yeye abaki huko mbinguni mpaka utakapofika wakati wa kurekebishwa vitu vyote, kama Mungu alivyosema kwa njia ya manabii wake watakatifu wa tangu zamani” (Matendo ya Mitume 3:20-21)! Wakati unakaribia ambapo Yesu Kristo atatawala duniani! Ujumbe huu, Injili ya Ufalme wa Mungu, ndio ule ambao Yesu alihubiri, na ni ujumbe wa kinabii! Unaweza kusoma baadhi ya unabii wa milenia katika vitabu vya Biblia vya Mika (Sura ya 4) na Isaya (Sura ya 2, 11 na 35)

Naam, unabii wa Biblia unatuambia kwamba ulimwengu utarejeshwa katika hali yake ya uzuri wa asili na usiochafuliwa na ustawi chini ya utawala mtakatifu wa Ufalme wa Mungu. Tunaweza kushangilia habari hii nzuri!

Kanisa Hai la Mungu linahubiri unabii wa Biblia, na linaweka wazi kueleweka kwake.
Kujua zaidi juu ya jinsi Mungu anavyotumia unabii kufunua mpango Wake, soma kijitabu chetu, Unabii Uliotimizwa: Mkono wa Mungu katika Mambo ya Dunia.

Copyright © 2009 Living Church of God
swahili.lcg.org